Tweet Share Share Share Share Share [video] Polepole atoa kauli ya CCM kuhusu uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika juzi. Unknown November 28, 2017 Soma zaidi » Siasa
Tweet Share Share Share Share Share Nape Atoa Neno kwa Vyama vya Upinzani Baada ya Uchaguzi wa Madiwani. Unknown November 28, 2017 Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, amekiri kuwepo na vitendo ambavyo siyo sahihi ambavyo vilivyojitokeza katika Uchaguzi wa marudio katika baadhi ya kata na kutaka hatua za kisheria zichukuliwe.Nape amefafanua hayo baada ya kuwepo na malalamiko hayo kutoka upande wa upinzani ambapo amesema kwamba vitendo hivyo vinapaswa kushughulikiwa kisheria kama wahalifu na siyo kushughulikiwa kisiasa na kwamba kufanya matendo hayo kisiasa ni njia za kuficha uovu.Pamoja na hayo Nape ameongeza kwamba hajawahi kuwa muumini wa matumizi ya nguvu kwenye siasa na wala hajawahi kushiriki mipango ya kutumia nguvu bali anaamini katika matumizi zaidi ya nguvu.Aidha Nape ameongeza kwamba sehemu zote alizofanya kampeni na wala hakubariki matumizi ya nguvu hivyo kuwashauri vyama vya upinzani wafanye tathmini ya kweli kisha kuchukua hatua pale walipoteleza katika uchaguzi."Rafiki zangu Upinzani fanyeni tathmini ya kweli halafu chukueni hatua pale mlipoteleza. Hichi kinachoendelea cha kutoa visingizio vya jumla. Sikatai kuwa kulikuwa na baadhi ya maeneo kumekuwa na vitendo si vya kibinadamu lakini si kwa kata zote. Vitendo hivyo vishughulikiwe specific kisheria kama wahalifu na si kushughulikiwa kisiasa".Amesema Nape Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, amekiri kuwepo na vitendo ambavyo siyo sahihi ambavyo vilivyojitokeza katika Uchaguzi wa marudio katika baadhi... Soma zaidi » Siasa
Tweet Share Share Share Share Share Magdalena Sakaya anena kuhusu kuondoka CUF. Unknown November 27, 2017 Naibu Katibu wa CUF Tanzania Bara, Magdalena Sakaya amedai hayuko tayari kuondoka Chama cha Wananchi CUF na kwenda katika vyama vingine hata kama chama chake kina mgogoro na iwapo na ikitokea Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ikiamua kukifutachama hicho yeye atastafu siasaAkifanya mahojiano maalumu na Nipashe, Sakaya amesema kwamba Mgogoro unaoendelea ndani ya chama chao ni wa Kikatiba na unafahamika kwa msajili wa vyama na kuongeza kama ikitokea kwamba CUF inafutwa basi yeye atastaafu siasa na siyo kuhama chama."Kwanza naamini CUF haiwezi kufutwa. Yaani hilo halipo pamoja na changamoto ya mgogoro iliyopo. CUF ina misingi yake na mgogoro uliopo ndani yake ni wa kikatiba. Kwa hiyo, mimi nikiamua kwamba sasa sitaki kuendelea kuwapo CUF, ninaacha siasa. Ninaendelea na mambo yangu mengine, eeeh" SakayaSakaya ameongeza kwamba "Kwanza mimi sijawahi kuwa na kadi ya CUF pekee. Nakumbuka wakati tunaripoti Shule yaSekondari ya Wasichana Kibosho (mwaka 1986) tuligawiwa kadi za kijani (CCM) wakati ule nchini kulikuwa na chama kimoja. Baadaye nikiwa na akili yangu timamu kadi niliyoichukua ni ya CUF ambayo niliichukua mwaka 1995 na ninayo mpaka leo na nitaendelea kuwa nayo. Naibu Katibu wa CUF Tanzania Bara, Magdalena Sakaya amedai hayuko tayari kuondoka Chama cha Wananchi CUF na kwenda katika vyama vingine hat... Soma zaidi » Siasa
Tweet Share Share Share Share Share Polepole amvaa Mbowe Unknown November 27, 2017 Chama cha mapinduzi CCM kimeibuka na ushindi katika kata 42 kati ya 43 zilizofanya uchaguzi mdogo wa udiwani jumapili ya Novemba 26 kwenye mikoa 19 nchini.Hayo yamebainishwa jana na katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Ndugu Humphrey Polepole, wakati akitoa tathmini ya uchaguzi mbele ya waandishi wa habari kwenye ofisi ndogo ya makao makuu ya chama hicho Lumumba jijini Dar es salaam.Polepole amesema kuwa Chama chake kimeibuka na ushindi huo katika kata hizo ikiwa ni matokeo ya kazi nzuri inayofanywa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya CCM.Polepole ameitaja kata ambayo chama chake kimekosa ushindi kuwa ni Ibigi iliyopo wilayani Rungwe mkoani Mbeya ambayo imechukuliwa na mgombea wa CHADEMA. Aidha Polepole amedai kuwa chama kimeumia kwa kuikosa kata hiyo lakini kimekubali matokeo.Kwa upande mwingine Polepole amezitaka mamlaka kushughulikia haraka baadhi ya dosari zilizojitokeza kwenye baadhi ya maeneo, ambayo chama hicho kimeripoti kutoridhishwa na mwenendo wa mchakato wa uchaguzi ikiwemo vitendo vya vurugu vilivyofanywa na watu wasiokuwa na nia njema. Chama cha mapinduzi CCM kimeibuka na ushindi katika kata 42 kati ya 43 zilizofanya uchaguzi mdogo wa udiwani jumapili ya Novemba 26 kwenye m... Soma zaidi » Siasa
Tweet Share Share Share Share Share Kafulila akabidhiwa kadi ya uanachama CCM. Unknown November 26, 2017 Hii ni baada ya kutangaza kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) siku ya Jumatano Davidi Kafulila na leo kukabidhiwa kadi ya uanachama ndani ya CCM.Kafulila alikabidhiwa kadi ya uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Katibu Mwenezi wa CCM, ndg Humphrey Polepole katika mkutano wa kumnadi mgombea wa udiwani wa chama hicho, kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani katika Kata ya Mbweni jijini Dar es salaam.Hapo awali Kafulila aliwahi kuwa mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kisha kufukuzwa na baadae kujiunga na Chama cha NCCR Mageuzi ambapo alifanikiwa kuwa Mbunge wa Kigoma Kusini mwaka 2010-2015 kwa tiketi ya chama cha NCCR Mageuzi na baadaye kurudi tena Chadema 2016 na hapo juzi jumatano alitangaza kukihama chama hicho kwa madai ya kuwa upinzani hauna nia ya kupambana na ufisadi.Kwa upande wa mkewe ambaye ni Mbunge Viti Maalumu kupitia chama cha CHADEMA, Jesca Kishoa juzi wakati akizungumza na wanahabari alipingana na kauli ya mumewe na kusema kwamba, mumewe anapaswa kusema ukweli na kwamba sababu alizozisema sizo zilizomuondoa ndani ya chama hicho huku akiongeza kwamba mume wake hana msimamo.Kafulila amekabidhiwa kadi hiyo ya CCM ikiwa imebaki siku moja kabla ya kuhitimishwa kwa kampeni za uchaguzi mdogo wa marudio ya nafasi za udiwani kwa Kata 43 ndani ya Tanzania. Hii ni baada ya kutangaza kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) siku ya Jumatano Davidi Kafulila na leo kukabidhi... Soma zaidi » Siasa
Tweet Share Share Share Share Share Lowasa asisitiza hana mpango wa kurudi CCM Unknown November 24, 2017 WAZIRI Mkuu wa Zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameweka wazi tuhuma za madai ya kurejea Chama Cha Mapinudizi (CCM).Juzi kupitia mitandao ya kijamii, kulikuwa na ujumbe wenye jina la Mrisho Gambo akidai amepokea ujumbe kutoka Monduli uliokuwa na ombi kubwa moja.Ujumbe huo uliokuwa umeandikwa kwenye ujumbe mfupi wa maneno, ulidai Mrisho ameombwa amuombee Mzee wa Monduli kwa Rais Magufuli ili akubali kumuona na yeye yupo tayari kurudi nyumbani kama rais atakubali kumuona.Akizungumza na mamia ya wananchi wa Kata ya Makabi katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru, wakati wa kampeni za kumnadi mgombea udiwani, Lowassa aliibuka na kudai hana mpango wowote wa kurejea CCM kama ilivyodai mitandao ya kijamii.Aliendelea kudai kwenye mkutano huo uliohudhuriwa pia na Mbunge wa Jimbo hilo, Nasari Sumari, kwamba taarifa hizo zinazodai kuwa kuna watu amewatuma kuomba arejee CCM, si za kweli zimelenga kupotosha umma.Lowassa ambaye amekuwa akizungumza kwenye maeneo tofauti kunadi wagombea wa udiwani Kanda ya Kaskazini, alisisitiza kwamba taarifa hizi zimejaa uongo wa kutunga.“Watu hawa wamekuwa wakitunga mambo mengi juu yangu, naomba niwaambie Watanzania sina mpango wala ndoto za kurudi CCM,” alisema Lowassa huku akishangiliwa na mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano huo.Lowassa aliyegombea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na kufanikiwa kupata kura zaidi ya milioni sita, aliendelea kueleza kwamba watu hao wamekuwa pia wakisambaza uongo watu kuzuiliwa na Serikali kumtembelea nyumbani kwake.“Yote haya ni maneno ya kutunga,” alisema Lowassa aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Monduli kabla ya kuhamia Chadema.Kwa nyakati tofauti, Lowassa ameshiriki mikutano ya kampeni za kuwanadi wagombea udiwani katika Kata mbalimbali zilizopo mikoa ya Arusha na Kilimanjaro.Akiwa mkoani Arusha tayari amefanya mikutano katika Kata ya Moita Bwawani wilayani Monduli, Murrieti jijini Arusha, baadaye akaelekea mkoani Kilimanjaro akiwa huko msafara wake ulijikuta ukirushiwa mabomu ya machozi kwa lengo la kutawanya watu waliokuwa wamemzunguka.Uchaguzi mdogo wa madiwani nchini unatarajiwa kufanyika Novemba 26, mwaka huu, baada ya madiwani waliokuwa wamepoteza sifa, huku wengine wakifariki na wengine kujiuzulu vyama vyao walivyokuwa wakivitumikia awali na hivyo kusababisha nafasi kuwa wazi. WAZIRI Mkuu wa Zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameweka wazi tuhuma za madai ya kurejea Chama ... Soma zaidi » Siasa